March 17, 2025 09:44:30 PM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Leo Ligi Kuu Tanzania Bara imefikia tamati kwa kushuhudia timu za Ruvu Shooting na Polisi Morogoro zikiipa mkono wa kwa heri ligi hiyo.
Matokeo ya mechi zote za leo yako kama ifuatavyo:
Azam FC 0-0 JKT Mgambo
JKT Ruvu Stars 1-2 Simba SC
Kagera Sugar 0-0 Tanzania Prisons
Mbeya City 1-0 Polisi Morogoro
Mtibwa Sugar 1-2 Coastal Union
Ndanda FC 1-0 Young Africans
Stand United 1-0 Ruvu Shooting
Kwa matokeo hayo, Ruvu shooting imebaki na pointi zake 29 huku Mgambo nayo ikifikisha pointi 29 sawa na Prisons iliyomaliza pia ikiwa na pointi hizo hizo 29 lakini Prisons na Mgambo zikiipiku Ruvu shooting kwa tofauti ya magoli.
Kwa upande wa Polisi Moro yenyewe iliendelea kubaki na pointi zake 25 baada ya kupoteza mchezo wa leo dhidi ya Mbeya City.
Hivyo timu 2 za mwisho katika msimamo wa ligi hiyo ni Polisi na Ruvu Shooting, wakati Stand, Mgambo, Ndanda na Prisons zikijinasua baada ya matokeo ya leo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
09 May 2015

Post a Comment

 
Top