Ikiwa kwenye misele ya mlala nje, ile Timu ya Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, imenasa tukio la aina yake ambapo mwanaume aliyejitambulisha kuwa ni mume wa mtu amekutwa na mwanamke changudoa akivaa suruali baada ya kuvunja amri ya sita ya Mungu kwenye eneo la biashara ya mamantilie!
Wakihamaki baada ya kukurupushwa.
Tukio hilo la aina yake lilinaswa kwenye uchochoro mmoja, maeneo ya Mwenge, Dar, majira ya saa 9:00 usiku ambapo wahusika hao ambao hawakutaka kutaja majina walikutwa wakiwa wanavunja amri ya sita kabla ya kushtuliwa na mwanga wa kamera za makachero wa OFM.
Wakiwa wanakatiza kwenye uchochoro huo, OFM walisikia miguno ya kimahaba ambapo ilibidi kutulia kidogo kujua kunani kinachoendelea mahali hapo.Waliposogelea waliwashuhudia wawili hao wakiwa wamevua nguo ambapo mwanamke alikuwa ametandika khanga chini bila kujali mtu anaweza kukatiza na kushuhudia sinema yao ya ngono.
Dada huyo akivaa baada ya fumanizi hilo.
Mara baada ya kuwafotoa picha kadhaa, wawili hao walishtuka huku mwanamke akivaa nguo harakaharaka kabla ya mwenzake naye kuvaa kisha wakataka kuanzisha timbwili kwa OFM.Wakati wawili hao wakizozana na OFM kwa kosa la kuwakatishia ‘mambo’ yao, alitokea jamaa mmoja aliyekuwa akilinda jirani na eneo hilo hivyo kuwapa woga wawili hao.
Hata hivyo, OFM iliwatisha kuwa eneo hilo siyo gesti wala ndani hivyo walichokuwa wakikifanya siyo sahihi ndipo wakajikuta wakiomba yaishe bila kurushwa gazetini.Kwa upande wake, mwanaume aliomba asamehewe akidai kuwa ni mume wa mtu na kama tukio hilo litaenda hewani itakuwa fedheha kwa familia yake.
“Huyu dada yeye hana shida sana kwani siyo mke wa mtu. Tatizo lipo upande wangu maana mkinitoa itakuwa fedheha kwa mke na watoto wangu,” alijitetea jamaa huyo bila kujua OFM walishakula kiapo cha kutokomeza uovu kwenye jamii.Baada ya aibu hiyo, wawili hao waliondoka mahali hapo na kutimkia kusikojulikana.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Wanafunzi wa Shule ya Msingi Wajiuza kwa Shilingi 2000 Wateja Wao Wakubwa ni Madereva Bodaboda21 May 20150
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Farao! Kumekuwa na madai ya baadhi ya wanafunzi wa shule ...Read more ?
- Pichaz: Pati 2 ya Padri wa Kanisa Katoliki Aliyenaswa Kichakani Akila Uroda na Kondoo Wake Jijini Dar19 May 20150
KISA cha Padri Anatoly Salawa (pichani) ambaye pia ana cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya ...Read more ?
- Pichaz: Wasanii Chipukizi wa Bongo Wanaswa kwa Ufuska Live..!18 May 20150
SHABAASH! ‘Makinda’ wawili wanao penyapenya katika sanaa ya maigizo runingani wa Kundi la San...Read more ?
- Fumanizi la Aina Yake......Padri wa Kanisa Katoliki Anaswa Kichakani Akila Uroda na Kondoo Wake Jijini Dar15 May 20150
KAMA mti mbichi unatenda haya, itakuwaje kwa mti mkavu?! Ndivyo inavyoweza kutafsiriwa kwa K...Read more ?
- Mwanaume Afumaniwa Gesti Na Mke Wa Rafiki Yake14 May 20150
Kashikashi za kuambiwa umefumaniwa zisikie kwa mwenzako tu! Utakuta mtu mkubwa, bonge, lakini ak...Read more ?
- Sharobaro, Hausigeli Wanaswa Live Sebuleni kwa Boss.....So Latinga Polisi06 May 20150
Kijana mmoja mtanashati, aliyefahamika kwa jina la Faraja Adam mkazi wa Makongo jijini Dar ...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment