March 16, 2025 07:44:30 PM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Muimbaji wa ‘Nobody But Me’ Vanessa Mdee a.k.a Vee Money ambaye hivi sasa ameweka wazi uhusiano wake na Jux ambaye ni boyfriend wake, ameweka wazi ni kipindi gani angependa kupata mtoto.

Vanessa (26) ambaye muziki wake umeanza kupata njia kwenye soko la kimataifa, amesema kuwa licha ya kuwa anapenda kupata mtoto lakini kwa sasa hayuko tayari kutokana na kuwa busy kupita kiasi.

“Sasa hivi sehemu ambayo nilipo katika maisha yangu niko very busy na kazi yaani, na nataka nikipata mtoto wangu au nikiwa tayari kupata mtoto niwe na uwezo wa kumlea sio kifedha tu lakini kuwepo katika maisha yake malezi ya mama yake ya karibu, akienda kulala nipo akiamka nipo kumchukua kutoka shuleni nipo, sasa hivi siwezi kufanya hivyo na siwezi kusema ndani ya miaka mitatu au minne mitano” Vee Money aliiambia Amplifaya ya Clouds Fm.


Alipoulizwa kama anampenda sana Jux alijibu, “Sana, he is a great guy…he is my boyfriend”

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
26 Apr 2015

Post a Comment

 
Top