Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Timu ya Sunderland imemtimua kocha wake Gus Poyet, hii ni kutokana na taarifa kutoka vyombo mbalimbali vya habari.
Kocha huyo mwenye uraia wa Uruguay ambaye amedumu kwa muda wa miezi 18 tu kwenye klabu hiyo, ametimuliwa kutokana na timu yake kutokuwa na matokeo ya kuridhisha hasa mara baada ya kupokea kipigo cha magoli 4-0 kutoka kwa Aston Villa juma lililopita katika uwanja wao wa nyumbani.
Siku ya kipigo hicho kuna baadhi ya washabiki wenye hasira walidiriki kutaka kumpiga baada ya kukasirishwa na matokeo hayo.
Ikumbukwe tu Sunderland mwanzoni mwa msimu huu walishawahi kufumuliwa vibaya na Southampton nyumbani kwao hapo hapo baada ya kukubali kipigo cha magoli 7-0.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top