Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
400103781475 
Tukio lililosikika leo kwenye Hekaheka ni ishu ya baba mmoja kumuunguza mtoto  wa jirani kama njia ya kuulipiza kisasi cha mtoto wake kuunguzwa kwa bahati mbaya wakati wakicheza na wenzake.
Mtoto huyo amesema alikuwa anatoka nje akiwa amebeba sufuria la moto, mtoto mmoja akatokea akiwa anakimbia na kugongana naye, mtoto huyo akaungua kwa bahati mbaya kichwani.
Baadae watoto walikuwa uwanjani wanacheza, baba wa mtoto aliyeunguzwa alimuita mtoto ambaye alimuunguza mwanae na kwenda naye nyumbani kwake, akaweka kisu jikoni na kumchoma nacho sehemu mbalimbali mwilini kama kulipiza kisasi.
Majirani baada ya kugundua tukio hilo waliamua kwenda kushtaki Serikali za mitaa kutokana na mama ambaye mtoto wake amechomwa kulipiza kisasi kuogopa kutoa taarifa akihofia kufukuzwa kwenye nyumba hiyo aliyopangishwa na baba ambaye kamchoma mwanae.
Polisi walifika eneo hilo na kumkamata mtuhumiwa.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top