Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
YANGA imetamka kuwa haina lengo la moja kwa moja kuachana na mshambuliaji wao Mrisho Ngassa na katika kuthibitisha hilo kwa vitendo, tayari uongozi wa klabu hiyo umeweka mezani Sh. 80 Milioni wakimtaka asaini dili jipya la kumbakisha timu hiyo.
Mmoja wa mabosi wa klabu hiyo aliyeko katika kamati ya usajili amesema kuwa uongozi wao chini ya mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji hauna nia ya kutaka kumtosa Ngassa ambapo tayari wameshampatia ofa hiyo kuhakikisha anasaini mkataba mpya.
Bosi huyo alisema katika ofa hiyo, Ngassa amepewa masharti mawili muhimu ambapo ametakiwa kutumia sehemu ya fedha hizo kumaliza deni lake la benki analodaiwa huku mshahara wake wa Sh. Mil. 4 ukibaki kama ulivyo.
Hata hivyo sharti hilo la mshahara linaenda tofauti na ofa ambayo Ngassa alitaka kupatiwa na klabu hiyo akitakia alipwe dola 3,500 (Sh. Mil 6.5) kwa mwezi ombi ambalo uongozi wa Yanga umeligomea.
“Hatuna nia ya kumuondoa Ngassa kuna vitu ambavyo anakosea, anaongea sana, haangalii kwamba juhudi zetu tunazozifanya tumeshampatia ofa hiyo afikirie sasa kama kweli anataka kubaki hapa,” alisema bosi huyo.
“Tumempa hiyo ofa lakini tatizo lake ni moja anataka mshahara mkubwa sana, kiasi ambacho ametaka tumpatie ni kikubwa sana kama atakuwa muelewa katika hili atakubali kusaini.”
Ngassa amekuwa akionekana kujuta kwa maamuzi yake ya kukataa ofa ye kwenda El Merreikh ya Sudan iliyomtaka wakati akiwa Simba kwa mkopo akitokea Azam ili tu akipige Yanga na kukumbana na adhabu ya kuwalipa Wekundu wa Msimbazi fedha alizosaini awali kabla ya kukimbilia Jangwani..
~udakuspecially

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top