Home
»
Matukio
» Baada ya Mwanaume Kukwepa Matumizi ya Mtoto Mke Ampa Kipondo Mumewe Mchana Kweupe Majirani Wapata Sinema ya Buree!
UPEPO umegeuka! Imani ya kwamba wanaume ndiyo wamekuwa wakiwapa kipondo wake zao imegeuka, safari hii mwanamke aliyejulikana kwa jina la Naomi Peter akimpa kipondo ‘hevi’ mumewe John Shila mchana kweupe!
Wawili hao wakazi wa Misheni, jijini Mwanza waliibua timbwili la aina yake ambalo liliwavuta watu wengi chanzo kikiwa ni mwanaume huyo kumkataa mtoto aliyezaa na mwanamke huyo.
Akizungumza na waandishi wetu, mmoja wa mashuhuda alisema wawili hao walioana na kuishi kama mke na mume na baadaye kupata mtoto mmoja wa kike, baada ya miaka miwili ulitokea ugomvi na kusababisha mwanamke kuondoka na ndipo John alipotumia mwanya huo kuoa mwanamke mwingine.
“Siku ya tukio, Naomi alimpeleka mtoto wake nyumbani kwa mzazi mwenzake kutokana na kutopewa hela ya matumizi, wakati huo Shila alikuwa na mwanamke wake mpya ndani, baada ya mabishano ya muda ndipo Naomi akaanza kumshughulikia Shila kwa kumtandika mangumi.
“Jamaa alikuwa hapeleki matumizi kwa mzazi mwenzie, mbaya zaidi alikataa na kudai mtoto si wake ndipo timbwili lilipoanzia,’’ kilisema chanzo hicho.
Chanzo hicho kilizidi kueleza kuwa, wakati ugomvi huo ukiendelea mwanamke wa John wa sasa alikuwa kimya ndani na kushuhudia mpenzi wake akipokea kichapo kisha kumkabidhi mwanaye amlee na yeye akaondoka zake.
Hadi shuhuda wa habari hizi anaondoka eneo la tukio, muafaka juu ya kilichofikiwa ulikuwa bado haujapatikana.
Credit: Gpl
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment