March 24, 2025 01:05:22 PM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Tuzo za muziki za Tanzania, Kilimanjaro Music Awards kwa mwaka 2015 zimezinduliwa rasmi.
IMG_9399

Meneja wa bia ya Kilimanjaro, Pamela Kikuli akiongea na waandishi wa habari

Uzinduzi huo umefanyika Jumatatu hii kwenye ukumbi wa mikutano wa jengo la LAPF jijini Dar es Salaam.
IMG_9409

Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA, Godfrey Ngereza

Akiongea na waandishi wa habari, meneja wa bia ya Kilimanjaro, Pamela Kikuli amedai kuwa zoezi la wananchi kupendekeza majina ya wasanii watakaowania tuzo hizo litaanza March 30 hadi April 19.
Tuzo za mwaka huu zina jumla ya vipengele 34.
IMG_9429
Wananchi watapendekeza majina hayo kwa kutumia tovuti, sms na whatsapp.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA, Godfrey Ngereza alisisitiza kuhusu umuhimu wa wasanii kujisali kwenye baraza hili kwakuwa mwakani hakuna msanii atakayehusishwa kwenye zoezi hili kama hatokuwa amejisajili.
IMG_9437

Meneja udhamini wa TBL, George Kavishe (kulia) akiongea na waandishi wa habari. Kushoto ni meneja wa Kilimanjaro, Pamela Kikuli

Naye meneja udhamini wa kampuni ya bia, TBL, George Kavishe alisema kuwa kwa mwaka minne sasa kasoro zilizokuwa zikijitokeza kwenye mchakato wa tuzo hizo likiwemo lile la wasanii kujiondoa zimepungua kwa kiasi kikubwa kwakuwa maboresho mengi yamefanikiwa pamoja na kutolewa elimu kwa wasanii.
IMG_9418

Alex Ofio wa Aim Group akionesha namna mbalimbali za wananchi kupendekeza majina kwenye tuzo hizo

Kilele cha tuzo hizo kimepangwa kuwa June 13 mwaka huu.
Source Bongo5

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
23 Mar 2015

Post a Comment

 
Top