Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Arsenal imefanikiwa leo hii March 14, 2015 kupata ushindi mzuri dhidi ya West Ham ikiwa ni mchezo wa ligi kuu uingereza msimu huu wa 2014/2015 wakati pia ikijiandaa kwa mchuano wa kata na shoka kati yake na klabu ya Monaco siku ya jumanne March 17,2015 kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Ulaya.

Kilabu hiyo ya Wenger iliishinda West Ham kwa mabao 3-0 na hivyobasi kujimarisha  katika nafasi ya nne bora katika msimamo wa ligi ya Uingereza.

The Gunner ilitawala mechi hiyo huku Olivier Giroud akifunga bao la kwanza kabla ya kipindi cha kwanza kukamilika.






Kevin Nolan na Matt Jarvis walikaribia kufunga kwa niaba ya wana nyundo hao lakini mabao ya dakika za mwisho ya Aaron Ramsey na Mathiew Flamini yaliiiweka Arsenal pointi nne mbele ya mabingwa wa zamani Manchester United walio katika nafasi ya nne.

Arsenal sasa inajianda kubadilisha matokeo ya 3-1 dhidi ya Monaco nchini Ufaransa siku ya jummane katika mechi ya vilabu bingwa barani Ulaya.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top