Home
»
Entertainment
» Ommy Dimpoz aelezea kosa alilofanya hadi kuzuiliwa uwanja wa ndege wa Marekani na kurudishwa Tanzania
Muimbaji wa ‘Ndagushima’ Ommy Dimpoz, weekend iliyopita alizuiliwa uwanja wa ndege wa Marekani, na kurudishwa Tanzania hivyo kushindwa kufika kwenye show aliyotakiwa kufanya Las Vegas weekend hiyo.
Dimpoz ameelezea mkasa mzima ulivyokuwa hadi kurudishwa nyumbani licha ya kuwa tayari alikuwa ametua Marekani.....
“Kilichotokea ni kwamba mi nilitoka hapa nikaenda mpaka Amsterdam, na Amsterdam nilikuwa naunganisha ndege kutoka Amsterdam kwenda Detroit na Detroit kwenda Vegas. Aliiambia Amplifaya ya Clouds Fm. “Kwahiyo kufika Amsterdam nilimiss flight ya connection ya kutoka Amsterdam kwenda Detroit ikabidi ni rebook booking yangu ili nipate flight nyingine ya kwenda Las Vegas.
Kwahiyo nikakosa ile connection ya kwenda Detroit ikabidi nipate connection nyingine kupitia Minnesota, nilivyofika kule ndege ambayo nilikuwa nimepata na connection niliyokuwa nimepata hii ya pili ikawa tayari imeshanichelewesha kwasababu nilitakiwa nifike usiku wa ile siku ya show, kwahiyo nikawa nimechelewa tayari, nikafika the next day.”
Aliendelea,
“Pale sasa kukawa kuna tatizo kule ikabidi wale watu wa siku ambayo walikuwa wameongea nao ilikuwa ni siku nyingine ikabidi waongee na jamaa kuwa jamaa amechelewa lakini tunaomba tufanye event next day, lakini jamaa wale wakakataa, na lengo ilikuwa mimi niperform kwenye hiyo weekend ya Rugby ile kama ulisikia alikuwepo Gyptian, Sauti Sol kwahiyo ilikuwa na mimi.”
Baada ya kufika uwanja wa ndege Marekani:
“Kwahiyo wakapiga simu (Uhamiaji) kule kwa wale watu wa event pamoja na venue, watu wa venue wakawaambia kulitakiwa kuwe na show hapa lakini msanii hakufika kwahiyo ikabidi waongee na promoter , promoters wakasema yah show tumeisogeza kwasababu msanii alichelewa alimiss flight. Sasa wakarudi kwangu wakaniambia lengo lilikuwa ni kwenda kwenye hiyo show na show tayari umeishai miss […] akasema kwamba lakini hapa unaonekana una show nyingine New York tarehe 21 nikawaambia ndio ilikuwa nikitoka Vegas naenda New York, wakaniambia sasa hii show ndio tunatatizo nayo kwasababu ni show ambayo inahusiasha chama cha kisiasa, na hata kama uliona kwenye promotion yangu ilikuwa nimeandika nitakuwa na show kwenye miaka 38 ya CCM Marekani […] kwahiyo wakaniambia kwamba hii Visa yako haikuruhusu wewe kuna aina ya visa nyingine ambayo unatakiwa uwe nayo ndo unaweza kuruhusiwa kuperform kwenye hiyo show.“
“Kwahiyo kwa kuangalia wakasema option iliyopo ni kwamba unatakiwa urudi nyumbani kwasababu shughuli ambayo ilikuleta imeshashindikana[…] Nikawaambia basi sawa mi nitarudi nyumbani, kwahiyo nasubiria tu sasa hivi promoter wale ambao waliandaa show ya Vegas wapange tarehe kwaajili ya hiyo venue ya show nyingine then ntaendelea na mchakato.”
Kwanini alichelewa ndege ya kuunganisha?
“Unajua nilishazoea kukaa zile connection za masaa matatu reporting time, kwahiyo pale nilijichanganya kwenye masaa […] kwahiyo katika kuangalia pale fikra zangu na mawazo nilishagazoea labda nimeunganisha kwenda D.C za kwenda L.A unakuta ukiunganisha unaweza ukakaa pale masaa matatu kufanya connection ya kwenda, lakini ile ilikuwa ni connection ya muda mfupi ni kama ya lisaa limoja kwahiyo mpaka ushuke utoke uende geti unalotakiwa kwenda, kwahiyo katika zile mishe mishe nikajikuta ile ndege mlango ishafungwa.”
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Diamond kuwania tuzo 5 za Afrima 2016, Alikiba na Yamoto Band moja08 Sep 20160
Diamond Platnumz ametajwa kuwania vipengele vitano kwenye tuzo za mwaka huu za Afrima. Vipeng...Read more ?
- Ujumbe wa Diamond kwa bintiye Wazua Gumzo......Kamwambia "Ukikua chonde mama ukitunze wasikile sana"23 Jul 20160
Diamond Platnumz si mgeni kwenye jumbe tata kwenye mitandao ya kijamii. Lakini ujumbe wake mpya...Read more ?
- Bifu Kali Kati ya Diamond na Clouds Media23 May 20160
Ni dhahiri sasa msanii wa kimataifa Diamond na brand kubwa ya radio na tv Clouds Fm, bifu la hadh...Read more ?
- Afande Sele Aungana Na Mbunge Joseph Msukuma Kuitaka Serikali Ihalalishe Matumizi Ya Bhangi02 Feb 20160
Msanii mkongwe wa hip hop nchini, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumiz...Read more ?
- Gari Jipya Analomiliki Masanja Mkandamizaji.10 Jan 20160
Msanii wa Vichekesho Anawakilisha kundi la Orijino Komedi anayejulikana kama Masanja Mkand...Read more ?
- Zari The Lady Boss Awakosha Mashabiki wa Penzi lake na Diamond Kwa Picha Hizi09 Jan 20160
Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ amewakosha mashabiki wa penzi lake na Diamond ‘Baba Tiffah’ baada...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment