Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendegu
**
OFISA Mtendaji wa kijiji cha Lumesule, Kata ya Lumesule, wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara, Swalehe Daimu, anadaiwa kupigwa na mkazi wa kijiji hicho, kwa madai ya kumkamata dada yake na kumtoza faini ya Sh 5,000 kwa kushindwa kushiriki shughuli za ujenzi wa maabara.
Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendegu, kijijini hapo jana, mlinzi huyo wa amani alisema kuwa tukio hilo limetokea Februari 4 mwaka huu, baada ya kuwakamata watu kumi kijijini hapo ambao hawakushiriki katika ujenzi wa maabara zinazoendelea kujengwa katika shule ya sekondari Lumesule.
“Sisi kama kijiji tumetunga sheria ndogo za usimamizi wa ujenzi huu, na mwananchi yeyote ambaye hakushiriki ni lazima akamatwe na kisha atozwe kiasi hicho cha fedha ili zisaidie kuendeleza ujenzi,” alisema.
”Baada ya kuwa nimewashikilia hawa watu na kuwafungia katika ghala la kijiji, huyo bwana alikuja kwa ajili ya kumlipia ndugu yake faini hiyo na kisha kunipiga vibao na kisha kunitishia maisha,” alifafanua Daimu.
Kwa mujibu wa mtendaji huyo, mtuhumiwa huyo amekuwa kikwazo kikubwa kwa shughuli za maendeleo kijijini hapo kwa kuwashawishi wananchi kutoshiriki shughuli za ujenzi wa maabara na miradi mingine ya maendeleo.
Akieleza tukio hilo, Daimu alilitupia lawama Jeshi la Polisi kwa kushindwa kumkamata mtuhumiwa licha ya kutoa taarifa kituo kikuu cha Polisi cha wilaya Mangaka, na kwamba mpaka sasa mtuhumiwa huyo yupo kijijini hapo , anaendelea kuwashawishi wananchi kukataa kushiriki ujenzi huo.
Kutokana na hatua hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Halima Dendego, ambaye yupo ziara ya ukaguzi wa maabara katika wilaya hiyo, alimwagiza Mkuu wa wa Wilaya kukamatwa haraka kwa mtuhumiwa huyo na kumfikisha mahakamani.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Uteuzi mwingine wa Rais Magufuli leo September 9 201609 Sep 20160
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo September 09 201...Read more ?
- Viongozi wa Afrika Mashariki Waigomea Ulaya....Wajipa Miezi Mitatu Kuutafakari Mkataba wa EPA09 Sep 20160
JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC), imeiomba Jumuiya ya Ulaya (EU), iipe muda wa miezi mitatu kuju...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Majibu ya Waziri mkuu Majaliwa Leo Bungeni kuhusu wahusika wa mauaji ya askari08 Sep 20160
Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inaendelea kukutana na wadau tofauti wanaohusika na ...Read more ?
- Makamu wa Rais: Viongozi Na Watumishi Wa Umma Kuchukuliwa Hatua Kali Iwapo Watabainika Kukiuka Taratibu Za Kazi08 Sep 20160
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameiagiza Sekretarieti ya M...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment