Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwizi aliyeiba gauni la muigizaji Lupita Nyong’o alilovaa kwenye tuzo za 2015 Oscars ameamua kulirudisha baada ya kugundua kuwa ni feki na halina thamani iliyotajwa.
lupita-nyongo-oscars-2015-2
Gauni hilo la Calvin Klein lililotengenezwa maalum kwaajili ya Lupita, lilimvutia mwizi huyo kulinyemelea na kuliiba baada ya kudaiwa kuwa na thamani ya $150,000 (zaidi ya shilingi milioni 274).
Lupita dress-2
Mwizi huyo aliwapigia simu mtandao wa TMZ na kuwaelekeza alipoliacha begi lenye gauni hilo, na TMZ walitoa taarifa polisi ambao walilifatilia na kulikuta limerudishwa hotelini lilipoibiwa lakini likiwa limewekwa bafuni chini ya sinki.
Lupita dress-1
Mtu huyo aliiambia TMZ kuwa aliliiba gauni hilo kwenye chumba cha Lupita baada ya kukuta mlango ukiwa wazi, na kubandua vigolori viwili na kuvipeleka kwa wataalam wambao walimwambia ni za bandia.
Mwizi huyo aliongeza kuwa aliamua kurudisha gauni hilo na kuwapigia simu TMZ ili kuumbua uongo wa mastaa wa Hollywood, na ulimwengu ujue kuwa gauni hilo halina thamani iliyotajwa.
~Bongo5

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top