March 19, 2025 10:41:46 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwanamke aitwaye Maria Haule  mkazi wa Kijiji cha Muhukuru Songea vijijini mkoani Ruvuma  ameuawa kwa kukatwa na shoka kichwani  na mume wake aitwaye  Salvatory Ndimbo  na kisha mwili wake  kuutupa mto Mkurumo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela anasema chanzo cha  mauaji hayo ni ugomvi  wa kimapenzi ambapo marehemu Maria Haule mwenye miaka arobaini  alikuwa na uhusiano wa kimapenzi  na mwanaume mwingine aitwaye  Anzekula na kutaka kuachana na  mumewe  Salvatory Ndimbo mwenye miaka sitini.
Jeshi la polisi linaendelea kumsaka mume wa  marehemu Maria Bw. Ndimbo mbaye ametoroka baada ya kufanya unyama huo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
23 Jan 2015

Post a Comment

 
Top