Mtoto mchanga mwenye umri wa mwezi mmoja, Yadiko Chigoda amelazwa katika Hospital ya Benjamini Mkapa Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma baada ya kupigwa na mchi kichwani na baba yake mzazi na kumsababishia maumivu makali.
Akizungumza mama mzazi wa mtoto huyo, Carolina Mnyawami ambaye ni mkazi wa kijiji cha Mingui kata ya Lumuma Wilayani Mpwapwa amesema tukio hilo limetokea leo majira ya saa 4 asubuhi ambapo mume wake aliyefahamika kwa jina la Fabian Chigoda alikuwa anapigana na kaka yake hivyo aliamua kuwaamulia ugomvi wao.
Amesema katika ugomvi huo walikuwa wanapigana na fimbo, hivyo alipowanyang’anya fimbo hiyo ili wasiendelee kupigana ndipo (Chigoda) alipoamua kuchukua mchi ili ampige nao mkewe kichwani lakini alikwepa na alipourusha ndipo ulipompata mtoto huyo kichwani.
“Nilipowanyang’anya fimbo ili wasiendelee kupigana, mume wangu aliokota mchi na kunirushia kichwani.. kwa bahati nzuri niliuona mchi huo na kukwepa ili usinipige ndipo ulipompiga kichwani mwanangu niliyekuwa nimembeba mgongoni,” amesema Carolina.
Ameongeza kuwa, “Baada ya kuona kuwa amempiga mtoto alikimbia na hajulikani alipo mpaka sasa.”
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Said Mawji amethibitisha kumpokea mtoto huyo na kwamba hivi sasa mtoto huyo anaendelea kupata tiba na uchunguzi zaidi wa afya yake.
“Ameumia sana kichwani lakini bado tunampatia tiba na uchunguzi zaidi kwenye fuvu la kichwa, kwani inaonekana kama vile limepasuka,” amesema Dk, Mawaji.
Hata hivyo amesema kuwa wanafanya mpango wa kumpa rufaa mtoto huyo ili aweze kwenda kutibiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mingui, Mwingwa Udoba amesema chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kifamilia na kwamba bado wanamtafuta baba mzazi wa mtoto huyo kwa kuwa alikimbia baada ya tukio hilo.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alipotafutwa kuzungumzia tukio hilo simu yake ilipokelewa na mtu aliyesema kuwa Kamanda alikuwa kwenye kikao cha kazi.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment