July 29, 2025 06:31:56 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Msanii wa filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ akipozi.
Stori: Gladness Mallya/Ijumaa Wikienda
BAADA ya hivi karibuni kumwagana na aliyekuwa mpenzi wake wa muda mrefu, Maximilian Bushoke, msanii wa filamu Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amefunguka kwamba hahitaji tena mwanaume kwa sasa.

Akipiga stori na paparazi wetu, Jini Kabula alisema kutokana na kwamba alikaa kwenye uhusiano wa kimapenzi muda mrefu na Bushoke na hakuona faida yoyote, anaujutia muda wake na sasa ameamua kuachana na masuala ya mapenzi na amejikita kwenye kazi zaidi.

“Nimegundua kwamba wanaume ni watu wanaonipotezea muda tu maana nilimsubiri Bushoke muda wote huo lakini alivyokuja Bongo akanipotezea hivyo nimeamua kujikita kwenye kazi zaidi,” alisema Jini Kabula.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
19 Jan 2015

Post a Comment

 
Top