Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
light_for_charlie1Mama mmoja mjamzito alikwenda Hospitali ya Mkoa Morogoro siku ya jana, alipofika hospitali hapo hakupata huduma nzuri kutoka kwa nesi aliyekuwa zamu, baada ya uchungu kumshika alihangaika bila msaada wowote na mwisho wake akajifungua chini.
Wakati huo ilikuwa usiku, umeme ulikuwa umekatika na wakalazimika kutumia tochi ya kwenye simu wakati akijifungua.
Nesi huyo alikuja kumpa msaada baadaye akamwambia kwamba tayari mtoto wake ameshafariki, hivyo awaite ndugu zake ili wamchukue mtoto huyo wakazike.
Ndugu walimchukua mtoto huyo akiwa amewekwa ndani ya  ndoo, walipofika nyumbani waligundua kwamba mtoto alikuwa mzima bado lakini waliporudi tena Hospitali jitihada za kumtibu hazikusaidia kwani alifariki wakati wakianza jitihada za kumshughulikia.
Mganga Mkuu Hospitali ya Mkoa Morogoro amesema kuwa hakuwepo kwa kuwa yupo likizo.
Isikilize hapa Hekaheka yote kwa kubonyeza play.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top