March 18, 2025 11:06:08 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
TV studio with camera and lights
Iwapo mtu anakuwa mtangazaji wa TV halafu ni mwanamitindo kuna namna ambavyo biashara zake zote mbili zikawa zinabebana, labda ndicho kilichomfanya avae nguo ambayo aliona itaonekana vizuri mbele za watu waliokuwa wakiangalia show ya TV ilipokuwa ikirekodiwa lakini kumbe kuna ambao hawakupenda hivyo.
Mtangazaji huyo Gauhar Khan hakutegema hili, limemkuta akiwa anarekodi sehemu ya mwisho ya show ya TV huko Mumbai, ambapo alitokea mtu mmoja Akil Malik na kumpiga kibao usoni na kusema kwamba Khan hakuvalia vazi sahihi kutokana na utamaduni wao kwani sketi yake ilikuwa fupi sana.
Haikuwa rahisi, Malik aliweza kukabiliana na walinzi zaidi ya mia mbili waliokuwa ndani na nje ya studio na  kuingia ndani ambapo alifanikisha lengo lake.
Jamaa huyo alikamatwa na kupandishwa kizimbani huku Khan akilazimika kurudisha ile mood ya kazi na kumalizia show hiyo japo alikuwa kwenye wakati mgumu bado kurudi kwenye hali ya kawaida.
Mkasa huo uko kwenye video hapa.
 kama kifaa chako hakina uwezo bonyeza hapa kuangalia video hiyo

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
13 Dec 2014

Post a Comment

 
Top