Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

 



Mhe. Anna Tibaijuka (Mb) na Waziri wa 62
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi shilingi bilioni 1.6.


 


Upande wa viongozi wa kisiasa ambao waliingiziwa fedha 
katika akaunti zao binafsi ni; Mhe.

Andrew Chenge (Mb)
Ndg. Daniel N. Yona ambaye alikuwa pia Waziri wa
 Nishati na Madini alipewa shilingi milioni 40.4. 

Ndg. Lucy L. Appollo ambaye ni Mtumishi wa TRA 
aliingiziwa shilingi milioni 80.8.

Ndg. Emmanuel Daniel Ole Naiko ambaye
alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa (TIC) aliingiziwa shilingi milioni
 40.4


 

Mhe.William Ngeleja (Mb) na ambaye alikuwa Waziri 
wa Nishati na Madini alipewa shilingi milioni 40.4


Ndg. Paul Kimiti ambaye ni Mbunge Mstaafu wa Jimbo la 
Sumbawanga
alipewa shilingi milioni 40.4


Dr. Enos S. Bukuku ambaye alikuwa Mjumbe wa Bodi 
ya TANESCO aliingiziwa shilingi milioni 161.7.


kwa upande wa Watumishi wa umma,Ndg. Philip 
Saliboko ambaye alikuwa mtumishi wa RITA aliingiziwa
shilingi milioni 40.4


Viongozi wa Madhehebu ya
Dini walioingiziwa fedha na Benki ya Mkombozi ni Askofu 63
Methodius Kilaini shilingi 80.9


Upande wa Majaji Prof. Eudes Ruhangisa, aliingiziwa
 milioni 404.25 na J.A.K Mujulizi aliingiziwa shilingi milioni 40.4


Mhe. Anna Tibaijuka (Mb) na Waziri wa 62
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi shilingi bilioni 1.6.

Mchungaji Alphonce Twimann Ye Simon shilingi milioni 40.4.

Askofu Eusebius Nzigirwa shilingi milioni 40.4

Watu walienda kugawana fedha kwenye Benki tajwa wakiwa na mifuko ya rambo, sandarusi,
mabox, magunia na lumbesa TegetaEscrow

Bilioni 73.5
zilitolewa na kugawanywa kwa watu mbalimbali kinyume cha
Sheria ya Benki Kuu na Taasisi za Fedha ya 2006 

Taarifa

ya benki (bank statements) yenye majina na akaunti zote
zilizoingiziwa fedha zimeambatishwa. 

Kamati imebaini mawasiliano kutoka kwa Katibu Mkuu
 wa Wizara ya Nishati na Madini na Katibu Mkuu Wizara ya
 Fedha
NA HAYA NDIO MAPENDEKEZO YA KAMATI

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AWAJIBISHWE KWA
 KUUDANGANYA UMMA WA WATANZANIA - MAPENDEKEZO YA 
KAMATI YA ZITTO

Filikunjombe: Kamati inashauri kuzitangaza benki za
 Stanbic na Mkombozi kama asasi za utakatishaji fedha

Filikunjombe: Kamati inashauri bodi ya Tanesco ivunjwe na 
TAKUKURU iwafungulie mashtaka ya rushwa.

Filikunjombe: Kamati imethibitisha kuwa Naibu waziri wa 
nishati na madini alisema uongo bungeni naye achukuliwe 
hatua.

Filikunjombe: Kamati imethibitisha kuwa Waziri wa 
Nishati na Madini Sospeter Muhongo amekuwa akisema
 uongo mara nyingi.

Filikunjombe: Kamati pia imethibitisha kuwa Waziri 
wa nishati na madini ndiye alikuwa dalali mkuu wa 
kuunganisha hawa watu

Filikunjombe: Kutokana na sababu hizo hapo juu, kamati 
inapendekeza kuwa Waziri wa Nishati na madini 
avuliwe madaraka yake.

Kamati inapendekeza kuwa uteuzi wa mwanasheria 
mkuu wa serikali utengeuliwe mara moja na 
aadhibishwe maana ametumia vibaya madaraka

Filikunjombe: Kamati pasipo mashaka imejidhihirisha kuwa 
Waziri mkuu alikuwa akijua jambo hili ila hakuchukua 
tahadhari.

Filikunjombe: alisema Mwalimu Nyerere kuwa kumbadili 
Waziri Mkuu sio jambo la ajabu.

Kwa vyovyote vile, Waziri mkuu anapaswa kuwajibishwa 
kwa namna yoyote ile ili kurudisha heshima ya 
serikali maana ameudanganya umma wa Watanzania kwa 
kusema uongo na kuitete kampuni hewa ya PAP isiyokuwepo

Filikunjombe: Kamati yetu inaamini kuwa Bunge hili 
litaitumia vizuri taarifa yetu hii

Mh. Spika anna Makinda amehairisha shughuli za Bunge na
 kusema kuwa kesho asubuhi serikali itatoa kauli zake.

Baada ya serikali kutoa kauli zake hapo kesho asubuhi, Wabunge wengine watapata nafasi ya kuchangia.


Credit Jamiiforums.com

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
29 Nov 2014

Post a Comment

 
Top