GOOD news kwa mtoto mzuri
Bongo Movies, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ ni kwamba anatarajia kuolewa hivi
karibuni baada ya kuishi maisha ya upweke kwa muda mrefu, Risasi
Jumamosi linakujuza.
Batuli ambaye ni mama wa watoto wawili, ameliambia Risasi Jumamosi
kuwa kwa umri alionao, amejifunza vitu vingi katika maisha hivyo kwa
kuwa ameshampata mtu sahihi kwake, ameona bora aolewe.
Alisema katika safari ya maisha, vikwazo ni vingi ikiwemo masuala ya
skendo za wasanii lakini ameshavuka vikwazo hivyo na hahitaji tena
kuyumbishwa na mtu kwani anaingia kwenye ndoa akiwa ameshajifunza mengi.
“Ndoa siyo kitu cha mchezo tena kwa sisi
wasanii mambo ni mengi. Kazi yetu tunakutana katika mazingira mbalimbali
hatarishi na wadau tofauti, vikwazo ni vingi na mtu akivuka salama basi
ni jambo la kumshukuru Mungu,” alisema Batuli.
Paparazi wetu alimbana zaidi Batuli ili aweze kujua hiyo ‘hivi
karibuni’ kwake ina maana ya lini ambapo hakutaka kutaja tarehe ya
harusi lakini akaahidi kumwanika mume wake mtarajiwa Desemba 5, mwaka
huu sambamba na kutaja siku husika ya ndoa.
“Wewe usijali, utakuwa wa kwanza kualikwa. Tena Desemba 5 nitakuita
umuone mume wangu mtarajiwa, nitakutambulisha kwa majina na kila kitu,
baada ya hapo nitakupa tarehe kamili ya ndoa yangu maana kila kitu
kimeshakaa kwenye mstari, soon tu nitakuwa mke wa mtu,” alisema Batuli.
Watoto wawili ambao Batuli anao kwa sasa, alizaa na wanaume wawili
tofauti ambao hapendi kuwazungumzia kwa kuwa tayari zama zao
zilishapita.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Diamond kuwania tuzo 5 za Afrima 2016, Alikiba na Yamoto Band moja08 Sep 20160
Diamond Platnumz ametajwa kuwania vipengele vitano kwenye tuzo za mwaka huu za Afrima. Vipeng...Read more ?
- Ujumbe wa Diamond kwa bintiye Wazua Gumzo......Kamwambia "Ukikua chonde mama ukitunze wasikile sana"23 Jul 20160
Diamond Platnumz si mgeni kwenye jumbe tata kwenye mitandao ya kijamii. Lakini ujumbe wake mpya...Read more ?
- Bifu Kali Kati ya Diamond na Clouds Media23 May 20160
Ni dhahiri sasa msanii wa kimataifa Diamond na brand kubwa ya radio na tv Clouds Fm, bifu la hadh...Read more ?
- Afande Sele Aungana Na Mbunge Joseph Msukuma Kuitaka Serikali Ihalalishe Matumizi Ya Bhangi02 Feb 20160
Msanii mkongwe wa hip hop nchini, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumiz...Read more ?
- Gari Jipya Analomiliki Masanja Mkandamizaji.10 Jan 20160
Msanii wa Vichekesho Anawakilisha kundi la Orijino Komedi anayejulikana kama Masanja Mkand...Read more ?
- Zari The Lady Boss Awakosha Mashabiki wa Penzi lake na Diamond Kwa Picha Hizi09 Jan 20160
Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ amewakosha mashabiki wa penzi lake na Diamond ‘Baba Tiffah’ baada...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment