Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Vijana wawili wakazi wa kata ya Sombetini jijini Arusha wamefariki dunia baada ya chumba walichokuwa wamelala kikiwa kimejengwa  kwa mabanzi kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia November 28  /2014.

Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha kamshna msaidizi Edward  Balele amesema uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa chanzo cha  moto ulipekelea vifo vya vijana hao Bw, Mohamed Katendela Juma na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Agaste ni mshumaa  waliokuwa  wanautumia kama nishati kwenye kibanda chao.
Kaimu kamanda Balele ameongeza kuwa pia uchunguzi unaonyesha  kuwa marehemu walikuwa na kawaida ya kutumia kilevi kupita kiasi  maelezo ambayo yamethibitishwa na baadhi ya majirani.
 
Wapangaji wa nyumba kilipojengwa kibanda hicho kilichoungua   wamesema kuwa vijana hao watoka kila siku  asubuhi kwenda kwenye  shughuli zao na kurudi  jioni  na mmliki wa nyumba na kibanda hicho ambacho hakina umeme Bi Sioni Leomoni amesema pia wana kawaida  ya kupika na kuvuta sigara ndani ya kibadna hicho.
Diwani wa kata ya Sombetini Bw Aally Bananga amesema pamoja na  ukweli kuwa ajali haina kinga lakini kuna haja ya kila mmoja kutimiza  wajibu wake wa kuchukua tahadhari juu ya mambo yanayoweza  kuhatarisha maisha yake na ya wengine.

CDT...ITV

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top