March 18, 2025 08:07:44 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan ametishia kuishtaki website iliyomtaja kama mmoja wa marais 10 wa Africa matajiri zaidi.
image
Mtandao huo uitwao. richestlifestyle.com umemtaja Jonathan kama rais wa sita kwa utajiri wake wa dola milioni 100
Maelezo kutoka ofisi yake yamedai kuingizwa kwake kwenye orodha hiyo hakuna ukweli na ni jaribio la kutaka kumuonesha kama fisadi
Tayari website hiyo imemuondoa kiongozi huyo wa Nigeria kwenye orodha.
Rais Jonathan amekuwa akikosolewa kwa kutotangaza mali zake hadharani.
Ikulu ya nchi hiyo ilitishia kuchukua hatua za kisheria hadi pale website hiyo itakapoitoa makala hiyo au kuomba radhi.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
10 Oct 2014

Post a Comment

 
Top