Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
 
 WASANII wa filamu nchini, Bond Bin Sinan na Salim Ahmed ‘Gabo’ hivi karibuni walinaswa wakisaga mirungi hadharani bila kujali kadamnasi.

Meza ya wasanii wa filamu Gabo na Bond ikiwa na dozi ya kutosha ya mirungi. Ishu hiyo ilitokea katika Ukumbi wa Dar West, Tabata Dar kulikokuwa na sherehe ya bethdei ya Wastara Juma ambapo wasanii hao walikuwa wamejaza mirungi kwenye mfuko wa nailoni na kuweka mezani huku wakitafuna kuanzia mwanzo hadi mwisho wa shughuli.
Gabo aking'ata mirungi. “Duh! Jamani hawa wasanii wanakula mirungi hapa ukumbini ambako kuna watu kibao na wa aina mbalimbali hawaoni kwamba wanavunja sheria za nchi?” alisikika mmoja wa waalikwa.

Wenyewe walipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, hawakuwa tayari kujibu lolote zaidi ya kuendelea kutafuna.
Bonyeza Hapa like ukurasa wetu wa facebook

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
06 Oct 2014

Post a Comment

 
Top