Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
MAHABAT! Kuonesha kwamba mahaba yamemkolea, staa wa Bongo Fleva, Snura Mushi ‘Mamaa Majanga’ amedaiwa kukacha shughuli za muziki na kutumikia penzi lake kwa mahaba motomoto.

Staa wa Bongo Fleva, Snura Mushi ‘Mamaa Majanga’ akiwa na mwandani wake, DJ Hunter.

Kudhihirisha hilo, chanzo chetu kimevujisha picha za mrembo huyo akiwa na mchumba wake anayefahamika kwa jina moja la DJ Hunter wakiwa katika malovee mazito kwa kupigana mabusu.

“Yani Snura sasa hivi muziki ameuweka pembeni anatumikia mahabati mwanzo mwisho,” kilidokeza chanzo chetu.

Meneja wa Snura, Mohamed Kavu ‘HK’.

Jitihada za kumpata msanii huyo kuzungumzia ukimya wake kwenye gemu hazikuzaa matunda lakini meneja wake, Mohamed Kavu ‘HK’ amekuwa akisisitiza kuwa msanii wake huyo yupo nchini Afrika Kusini katika shughuli za kimuziki huku pia kukiwa na madai kuwa msanii huyo ni mjamzito tarifa ambazo pia zinakanusha na HK.

Kibonajoro.com ndio mtandao wako kwa habari za ndani na nje, Tuwe pamoja huku pia >> Facebook

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top