Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Fatma Leonard 'akila kona'.
MSANII wa filamu Bongo, Fatma Leonard wiki iliyopita alinaswa na paparazi wetu akihamisha vitu vya ndani nyumbani kwa mpenzi wake huko Ubungo Makuburi jijini Dar es Salaam akidai kuchoshwa na maisha bila ndoa. Hata hivyo, paparazi lilikuta tayari mzigo wa fenicha umeshaondoka.
Msanii wa filamu Bongo, Fatma Leonard akifungasha virago kuianza safari.
“Nimemvumilia kwa muda mrefu sana, kila siku namkumbusha, sasa inaonekana kama ninalazimisha, nimeamua kuchukua vyangu kwa sababu nimempata mtu mwenye mapenzi ya kweli ambaye yupo tayari kunioa,” alisema Fatma akikataa kulitaja jina la mpenzi wake huyo anayempotezea muda.
Baba mwenye nyumba hiyo alimpigia simu mpangaji wake kumfahamisha kuhusu kuondolewa kwa mizigo hiyo, lakini alimtaka amuache achukue anachotaka, kitu kinachoonyesha aliridhia kitendo hicho kilichowavutia majirani wengi waliojazana kushuhudia.
Bonyeza Hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
27 Aug 2014

Post a Comment

 
Top