Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum
Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad
Mussa Salum (pichani kushoto), amewavaa baadhi ya mastaa Waislamu wa
Kibongo wenye kaunta zenye pombe majumbani mwao hasa kwa kipindi cha
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani huku akiwataka waondoe mara moja kwani ujana
unawasumbua, Ijumaa lina ripoti kamili.
WAMO DIDA, WEMA & DIAMOND
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba baadhi ya mastaa Waislamu
wenye kaunta zenye pombe majumbani mwao kuwa ni pamoja na Mtangazaji wa
Radio Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’, staa wa sinema za Kibongo, Wema
Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul
‘Diamond Platnumz’.
Akizungumza na Ijumaa mapema wiki hii jijini Dar es Salaam, Shehe
Salum alisema kwamba, kwanza ameshtushwa na habari ya hao wanaojiita
mastaa kuwa na kaunta za pombe majumbani kwao kwani ni habari ngeni
masikioni mwake na kusema kuwa kwa semina wanayoipata mwezi huu
hawatakiwi kutenda maovu.
Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
WANAPASWA KUOMBA DUA
Alisema kuwa mastaa hao wanapaswa kuutumia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kusoma Quran, kuomba dua na kuacha maovu yote.
“Hao mastaa wenye kaunta wanatakiwa kuacha
na kuondoa kabisa kwani Ramadhani imeletwa kwetu kama semina na
hatutakiwi ikiisha turejee kule tulipokuwa.
“Mafunzo ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani maana yake tujifunze na
tuachane na kule tulikotoka, hivi kwa nini wasijiulize mastaa wenzao
wako wapi kwa mfano Sharo (mchekeshaji Sharomilionea) na wengine
waliotangulia mbele ya haki?
WANAKULA UJANA?
“Wasijidanganye na ujana walio nao, wakikutwa na mauti, mbele ya haki watasema nini?
“Nawaasa kutorudi nyuma na kujifunza kwelikweli namna ya kuishika dini na nguzo zake,” alisema shehe huyo.
Baa ya ndani ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
SWAUMU ZAO VIPI?
Shehe mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake anayeswalisha katika msikiti uliopo Sinza jijini Dar alisema:
“Kiukweli kabisa pombe ni haramu na
hatutakiwi kuikaribia hata kidogo. Hawa ambao wamefikia hatua ya kuwa
na kaunta za pombe majumbani kwao, wanakosea sana.
“Kwa mfano mwezi huu mtukufu kama wanafunga, si kwamba hawapati
thawabu, wanapata ila kwenye kuikaribia pombe, watakuwa wanapata
dhambi. “Kwa hiyo unaweza kuwa umefunga lakini ukashangaa mpaka mwezi
umeisha thawabu zako zimepungua kutokana na mambo mengine yanayokufanya
upate dhambi.”
Mtangazaji wa Radio Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’,
DIDA ANASEMAJE?
Baada ya Shehe Salum kuwavaa mastaa hao, gazeti hili lilimsaka mmoja baada ya mwingine.
Alipopatikana, Dida ambaye ni binti wa
Kiislamu mwenye kaunta ya pombe nyumbani kwake, Mwananyama, Dar alikuwa
na haya ya kusema:
“Ni kweli mimi nina kaunta ndani kwangu lakini kwa mwezi huu hata
mimi naichukia sana pombe na sipendi kabisa kuiona pamoja na kwamba
sijui sana sheria za dini japo ni muhimu kuzijua nguzo zake.“Hata mimi
kama binti wa Kiislamu kwa mwezi huu mtukufu sinywi pombe na hiyo kaunta
ni kwa ajili ya wageni wangu wanaonitembelea.”
Staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’
NYUMBANI KWA DIAMOND
Wiki mbili zilizopita ishu hiyo ilitibua
futari nyumbani kwa Diamond maeneo ya Sinza-Mori, Dar hivyo kulazimika
kuondoa pombe kali zilizokuwa zimejazwa kwenye kaunta.WEMA VIPI?
Kwa upande wake Wema ambaye ukiingia kwake
kitu cha kwanza unakutana na kaunta ya pombe na vinywaji vingine
alipotafutwa ili kuzungumzia ishu hiyo, simu yake ya kiganjani iliita
bila kupokelewa.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment