Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Mwanaume aliyesutwa akilishwa keki na Maimartha.
WERAA! Watu weweee! Dume lililofahamika kwa jina moja la Lusajo au Sajo anayefanya kazi maeneo ya Kijitonyama, Dar jirani na duka la mtangazaji Maimartha Jesse ‘Mai’ amejikuta akitaharuki na kuaibika baada ya kusutwa laivu katikati ya wanawake huku akilishwa keki na kufunguliwa mvinyo kisa umbeya, Ijumaa Wikienda limeshuhudia tukio zima.


Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa eneo la tukio wikiendi iliyopita kabla ya gazeti hili kutua, Maimartha alidaiwa kusuka ishu hiyo huku akiwakaribisha marafiki zake kushuhudia akiwemo Flora Mvungi.
 Ilisemekana kwamba Mai alidai kuwa kilio chake kwa muda mrefu ni kwamba jamaa huyo amekuwa akimfuatafuata na kumwambia mumewe, Raymond Shayo ‘Shaa’ kila jambo analolifanya dukani hapo, ikiwa ni pamoja na kumweleza watu wa kila aina wanaoingia ndani hapo.
Maimartha akifungua Shampeni
 “Nilishapata taarifa za Sajo kuwa huwa ananichunguza, sikutaka kuwa na haraka nikaenda naye taratibu bila kumwambia kwani nilikuwa nikimtafutia dawa ya kumkomesha. Leo ndiyo arobaini yake imefika.
 “Nilishika simu ya mume wangu nikakuta SMS za Sajo zikimuomba fedha, ukweli nilichukia sana na nilishangaa kuona kumbe kazi anayoifanya ya kunichunguza analipwa, nikaona sasa ndiyo wakati wa kumkomesha kwani kwa kulipwa kwake ipo siku atatunga hata uongo kwa sababu fedha ni shetani,” alisema. 
 Keki ya msuto aliyoandaliwa Bw. Sajo.
Lusajo, 'Sajo' akihojiwa na Gea.
Sajo, kabla ya kujua kinachoendelea, alikaribishwa keki na shampeini, akaenda kichwakichwa, alipomaliza kulishwa akaambiwa asome maneno yaliyoandikwa kwenye keki ‘Sajo acha umbeya ndoa  tamu’ ndipo akachanganyikiwa na moja kwa moja msuto ukaanza huku akiulizwa ni kwa nini anamwambia maneno mume wa Mai.
Baadhi ya wadau walioalikwa na Maimartha kumsuta Bw. Sajo kwa umbea.
“Mh! Mimi mbona siyo kweli jamani,”  alisema Sajo na kushindwa kumalizia maneno. 
Alipobanwa na wanahabari wetu na Gea Habibu (wa Leo Tena ya Clouds FM) juu ya kuwa na namba ya simu ya mume wa Mai, Sajo alishikwa na kigugumizi na kuondoka ambapo alikimbilia dukani kwake na kujifungia kukwepa aibu kwani siyo tukio la kawaida kwa mwanaume kusutwa kwa umbeya.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
 
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top