Jeshi la Marekani limefanya
shambulizi la makombora dhidi ya mtu anayeshukiwa kuwa mmoja wa viongozi
wa kundi la wanamgambo la al-Shabaab nchini Somalia.
Al-Shabab linasemekana kuwa na uhusiani na kundi la kigaidi la Al-Qaeda.
Taarifa kutoka katika makao makuu ya ulinzi nchini Marekani zinasema kuwa mlengwa katika shambulizi hilo ni kiongozi wa makundi mawili ya kigaidi.
Mmoja wa viongozi wa al shababaab anaseama kuwa mshukiwa alikuwa Sahal Iskudhuq, kamanda mmoja wa al-Shabaab ambaye alikuwa na uhusiano wa karibu sana na kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeeda.
Hata hivyo hakuna uhakika ikiwa mshukiwa huyo ameuawa.
Marekani iliwahi kufanya shambulizi ambalo lilitibuka dhidi ya mmoja wa viongozi wa kundi hilo katika eneo la Barawe - linalosemekana kuwa ngome kuu ya Al Shabaab mwezi Oktoba.
Al Shabaa waliohusika na mashambulizi ya kigaidi katika jengo la maduka la Westgate, limedhoofishwa na mapambano dhidi yao kutoka kwa wanajeshi wa Muungano wa Afrika
Kusini na Kati mwa Somalia.
Marekani nayo imejitolea sana kukabiliana na kundi hilo kwa kutuma kikosi cha ushauri wa kijeshi mjini Mogadishu.
Source:bbcswahili
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment