Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Mtu mmoja mjini Alabama nchini Marekani amefungua kesi ya madai baada ya kudai kuwa alikwenda kutahiriwa lakini madaktari wakaondoa uume wake wote.


Tovuti ya Metro imesema Johnny Lee Banks Jnr anadai kuwa alikwenda kufanya 'suna' katika hospitali ya Princeton Baptist Medical Center na uume wake kukatwa kimakosa na madaktari.


Kesi hiyo iliyofunguliwa na Bwana Banks pamoja na mkewe Zelda, inasema bwana huyo hakupewa maelezo yoyote ya kwanini 'mashine' yake iliondolewa na wala hakuonywa kuwa shughuli ya kutahiri ina hatari na uwezekano wa kukatwa kabisa uume.


"Mshtaki alipozinduka kutoka kwenye dawa ya usingizi baada ya upasuaji, alikuta uume umekatwa," yamesema maelezo ya mashtaka.


"Mdai hakutoa idhini yoyote ya kukata kabisa au nusu ya uume wake,' imesema karatasi ya mashtaka. 


Bwana huyo ameitaja hospitali, pamoja na madaktari wawili kuwa ndio washtakiwa katika kesi hiyo, akisema walikuwa wazembe na walishindwa kutafuta msaada walipopatwa na tatizo wakati wa upasuaji.

Chanzo Bonyeza hapa

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top