Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

taliban1


Maafisa nchini Afghanistan wanasema kuwa watu 11 wamefariki akiwemo mwangalizi mmoja wa uchaguzi baada ya gari lao kaskazini mwa taifa hilo kukanyaga bomu lililotegwa barabarani siku moja tu baada ya kuanza kwa uchaguzi wa urais wa raundi ya pili.Katika tukio jengine kundi la Taleban limewakata vidole baadhi ya raia kama adhabu ya kushiriki katika uchaguzi nchini humo.


Zaidi ya watu 60 wameuawa na wanamgambo hao katika misururu ya mashambulizi wakati wa raundi ya pili ya uchaguzi wa urais.

taliban
Raia wa taifa hilo wanachagua kati ya aliyekuwa Waziri wa mambo ya kigeni Abdulla Abdulla na Ashraf Ghani ambaye aliwahi kuwa waziri wa fedha.
Wagombea wote wameahidi kuimarisha uhusiano na mataifa ya magharibi mbali na kukabiliana na ufisadi.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top