Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
UN yaiweka Boko Haram katika orodha ya magaidi 
Umoja wa Mataifa umeliweka kundi la Boko Haram la nchini Nigeria katika orodha ya makundi ya kigaidi sambamba na kuwawekea vikwazo viongozi wa kundi hilo.

 Hatua hiyo ilichukuliwa hapo jana na imekaribishwa pia na wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kutaka kuanza utekelezwaji wa vikwazo hivyo mara moja. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, vikwazo hivyo vinahusu kuuziwa silaha kundi hilo, kufungwa akaunti za fedha sambamba na kuzuiwa kufanya safari viongozi wa kundi hilo.
 Hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni baada ya mwezi mmoja tangu kundi hilo lilipowateka nyara wanafunzi wa kike, suala lililoibua makelele ya ndani na nje ya nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika. Zaidi ya wanafunzi 200 wa shule ya sekondari wa Chibok ulioko kwenye jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo walitekwa nyara tarehe 14 Aprili mwaka huu na kundi hilo ambapo 53 kati yao walifanikiwa kutoroka.

<<<<Bofya hapa ulike page yetu>>>>


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top