Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Wanafunzi walitawanywa kwa kutumia gesi ya kutoa machozi


Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Kenya wamezua vurugu wakipinga mpango wa serikali kutaka kuongeza karo katika vyuo vikuu vyote vya umma. 
Polisi walipambana na wanafunzi hao kwa kutumia gesi ya kutoa machozi kutawanya wanafunzi hao ambao walizua vurugu mjini na kuwapora abiria huku wakiharibu magari ya umma na yale ya abiria katika barabara kuu ya Uhuru katikakati ya jiji la Nairobi.




Alisema kuwa ripoti kuwa karo itaongezwa sio sawa na ni za kupotosha akisisitiza kuwa ikiwa jambo kama hilo litafanyika litahitajika kutangazwa na baraza la vyuo vikuu nchini humo baada ya makubaliano kufikiwa. 
Wanafunzi hao wanapinga mpango wa serikali wakisema kuwa kuambatana na mfumuko wa bei, karo yao haipaswi kuongezwa na kwamba serikali inapaswa kushauriana nao kabla ya kufikia hatua zozote za kuongeza karo.
Wanafunzi watano wameripotiwa kujeruhiwa katika vurugu. 
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>> 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top