
Wanafunzi walitawanywa kwa kutumia gesi ya kutoa machozi
Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini
Kenya wamezua vurugu wakipinga mpango wa serikali kutaka kuongeza karo
katika vyuo vikuu vyote vya umma.
Polisi walipambana na wanafunzi hao kwa kutumia
gesi ya kutoa machozi kutawanya wanafunzi hao ambao walizua vurugu
mjini na kuwapora abiria huku wakiharibu magari ya umma na yale ya
abiria katika barabara kuu ya Uhuru katikakati ya jiji la Nairobi.
Pia waliripotiwa kuvunja maduka na kuharibu mali ya watu.
Wachuuzi walilazimika kuondoka mjini huku polisi
wakipambana na wanafunzi hao ambao waliungana kutoka vyuo vikuu mbali
mbali kote nchini Kenya.
Awali maandamano yao yalikuwa salama ingawa
baadaye wanafunzi hao walioanza kuandamana tangu saa nne asubuhi
walianza kuzua rabsha na kulazimisha polisi kutumia mabomu ya kutoa
machozi kuwatawanya.
Wanafunzi hao wanaandamana kupinga mapendekezo
ya serikali kuongeza karo ya vyo vikuu , ingawa waziri wa elimu ya juu
Profesa Jacob Kaimenyi amesema kuwa serikali bado haijatoa tamko rasmi
ikiwa wanafunzi wa vyuo vikuu watalazimika kuongeza karo.
Alisema kuwa ripoti kuwa karo itaongezwa sio
sawa na ni za kupotosha akisisitiza kuwa ikiwa jambo kama hilo
litafanyika litahitajika kutangazwa na baraza la vyuo vikuu nchini humo
baada ya makubaliano kufikiwa.
Wanafunzi hao wanapinga mpango wa serikali
wakisema kuwa kuambatana na mfumuko wa bei, karo yao haipaswi kuongezwa
na kwamba serikali inapaswa kushauriana nao kabla ya kufikia hatua
zozote za kuongeza karo.
Wanafunzi watano wameripotiwa kujeruhiwa katika vurugu. <<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro











Post a Comment
Post a Comment