Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
pakistan2
Mume wa mwanamke wa nchini Pakistan aliyepigwa mawe hadi kufa Farzana Parveen, kwa kukataa kushiriki katika mipango ya ndoa na mwanaume aliyechaguliwa na familia yake amesema kuwa alimuua mke wake wa kwanza ili aweze kufunga ndoa na ParveenMwanaume huyo Mohammad Iqbal, 
 
amesema kuwa alitaka kuwasilisha maombi yake kwa Parveen hivyo aliamua kumuua mke wake kwanza ambapo mamlaka za nchini Pakistan zimesema mke huyo wa kwanza aliuwawa miaka sita iliyopita.Alikamatwa na polisi na baadae kuachiwa kwa dhamana kwasababu mtoto wake wa kiume alimsamehe kutokana na kitendo hicho.

Mtoto wake wa kiume ambaye kwa wakati huo alikuwa na umri wa miaka 20 amethibitisha taarifa hizo na kusema baba yake alitumikia kifungo cha mwaka mmoja gerezani.
Parveen ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi mitatu alipigwa mawe hadi kufa na kundi la watu wakiwemo kaka zake, baba yake na ndugu wa familia yake Mashariki mwa mji wa Lahore ambapo waziri mkuu wa Pakistan Nawaz Sharif amemtaka waziri wa Jimbo hilo kuwasilisha maelezo juu ya tukio hilo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top