
Bila
shaka mashabiki wa Diamond Platnumz watakuwa na shauku kubwa ya
kufahamu codes za kumpigia kura staa huyo aliyetajwa kuwania tuzo za BET
mwaka huu kwenye kipengele cha Best International Act: Africa, kama
ilivyo katika tuzo zingine.Habari
mbaya ni kuwa hakuna codes zozote zitakazotolewa kwakuwa tuzo hizo zina
utaratibu tofauti kabisa na tuzo zingine kama CHOAMVA ama MTV MAMA. Ili
kupata washindi, tuzo za BET huwa ina jopo la watu 500 duniani (academy
member) ambao huchagua mshinda katika vipengele vyote.
Habari njema ni kuwa, Vanessa Mdee pia ni
miongoni mwa member wa academy hiyo ambayo hakuna shaka kuwa atampa
Diamond kura moja kama alivyosema: “Y’all already know where my vote
went.”
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment