Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Milipuko miwili mikubwa imetokea nchini Nigeria katika mji wa Jos.
Milipuko hiyo imetokea katika soko ambalo lina shughuli nyingi na ambalo lilikuwa na msongamano wa watu eneo la Kati mwa Nigeria.
Mwandishi wa BBC Ishaq Khalid aliye mjini humo anasema kuwa kuna hofu ya watu wengi kujeruhiwa hasa kwa kuwa soko hilo lilikuwa na idadi kubwa ya watu.
Haijulikani kilichosababisha milipuko hiyo mjini Jos, mji ambao umeshuhudia mashambulizi makali kati ya wakristo na waisilamu.
Kundi la Boko Haram, pia limekuwa likifanya mashambulizi katika mji huo.
Chanzo bbcswahili
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top