Mitaa
mbalimbali nchini Brazil imekua ikitajwa kwa uhalifu kutendeka mara kwa
mara hata wakati wa mchana lakini pia vilevile wizi huo umekua
ukifanyika hata kwenye maeneo ambayo mgeni yeyote anaweza kuamini ni
maeneo salama kutokana na ustaarabu unaoonekana lakini pia wingi wa
watu.
Hii
video hapa chini ni ya mama aliekua akihojiwa kwenye TV lakini ghafla
akatokea mwizi na kutaka kupita na mkufu wake wa gold, mkufu huo haukua
rahisi kunyofoka hivyo mwizi akakimbia na mikono yake mitupu.
Yani wezi kuibia watu ovyoovyo tu town imekua ni kitu cha kawaida kabisa kama inavyoonekana kwenye hii video hapa chini.
Hili
ni onyo kwa mashabiki watakaokwenda Brazil kwa ajili ya kushuhudia
mechi za kombe la dunia, unaambiwa mwezi uliopita Polisi wa Brazil
wapatao 1400 wakiwa na magari maalum pamoja na msaada wa helikopta
walivamia na kusafisha moja ya sehemu zinazoaminika kuwa na wezi wengi.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment