![]() |
| Kamanda Ahmed Msangi. |
Mkazi wa kijiji cha Itimba wilayani
Mbeya, Happy Petter (16) anashikiliwa na polisi kwa kumpiga mtoto wa
kufikia na kumsababishia kifo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani
Mbeya, Ahmed Msangi mtoto huyo Francis Maneno (2) alifariki dunia wakati
akiendelea kupata matibabu katika hospitali ya rufaa Mbeya.
Kamanda Msangi alisema Francis
alifikishwa hospitalini hapo akitokea kijijini kwao Itimba kutokana na
majeraha aliyokuwa nayo mwilini yaliyosababishwa na kipigo alichokipata
kutoka kwa mama yake wa kambo.
Alisema Aprili 4 saa 2:00 asubuhi mama
huyo alimpiga mtoto sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia
majeraha ambapo chanzo cha kipigo hicho hakijafahamika.
Katika tukio jingine mwanafunzi wa darasa
la pili katika shule ya msingi Chapwa katika mji mdogo wa Tunduma
wilayani Mbozi Blanda Charles (9) amekufa baada ya kuzama katika mto
Chapwa wakati akiogelea.
Alisema mwili wa mwanafunzi huyo uligunduliwa na mmoja wa wapita njia, Kapanda Chisunga alipokuwa akivuka mto huo.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment