Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani John Kerry akizungumza na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov.
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani amelaumu Urusi kwa kuchochea mapigano Mashariki mwa Ukraine.
John Kerry alisema ujasusi wa Marekani una hakika kuwa Urusi imetoa silaha na wapiganaji na pia inaendelea kugharamia na kusimamia wapiganaji wa nchini Ukraine kushiriki ghasia hizo.

Katika lugha ya hasira, Bwana Kerry, alishambulia Urusi akisema kuwa taifa hilo limeshindwa kuchukua hatua madhubuti za kujaribu kutuliza uhasama ulioko nchini Ukraine kama ilivyokubaliwa mjini Geneva juma lililopita.

Bwana Kerry alisema kuwa Urusi inasimamia ghasia zinazoendeshwa na watu wanaotaka kujitenga kutoka kwa Ukraine Mashariki mwa taifa hilo na kujaribu kusababisha ghasia ili kuhujumu uchaguzi unaotazamiwa kufanywa mwezi ujao.

Kwa hasira, Bwana Kerry alilaumu Urusi kwa ghasia zote zinazoendelea Ukraine wakati huu. Ingawa hakutangaza vikwazo inavyoweza kuongezewa Urusi Bwana Kerry alisema mwanya wa kuimarisha amani katika Ukraine unaendelea kuziba.
>>>>bbcswahili
<<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU PLEASE>>>>>>

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top