Katika lugha ya hasira, Bwana Kerry, alishambulia Urusi akisema kuwa taifa hilo limeshindwa kuchukua hatua madhubuti za kujaribu kutuliza uhasama ulioko nchini Ukraine kama ilivyokubaliwa mjini Geneva juma lililopita.
Bwana Kerry alisema kuwa Urusi inasimamia ghasia zinazoendeshwa na watu wanaotaka kujitenga kutoka kwa Ukraine Mashariki mwa taifa hilo na kujaribu kusababisha ghasia ili kuhujumu uchaguzi unaotazamiwa kufanywa mwezi ujao.
Kwa hasira, Bwana Kerry alilaumu Urusi kwa ghasia zote zinazoendelea Ukraine wakati huu. Ingawa hakutangaza vikwazo inavyoweza kuongezewa Urusi Bwana Kerry alisema mwanya wa kuimarisha amani katika Ukraine unaendelea kuziba.
>>>>bbcswahili
<<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU PLEASE>>>>>>
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment