
Katibu
Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru
wadhifa huo kuanzia Aprili mwaka huu kutokana na mkanganyiko wa uongozi
ndani ya chama hicho.
Mwampiki
amesema amechoshwa na marumbano ya mara kwa mara na meza kuu ndani ya
chama hicho katika ngazi ya wilaya hivyo kudhoofisha juhudi zake za
kukijenga chama hicho.
Aidha Mwampiki amesema viongozi wa chama hicho wamekuwa na marumbano ya
mara kwa mara hivyo yeye kama kiongozi hayupo tayari kuona mambo
yanavurugika katika chama hicho.
Hata hivyo katika uamuzi aliouchukua Lucas Mwapiki amesema kuwa yeye
atabakia kuwa mwanachama wa chama hicho na Diwani wa Kata ya Mwakibete
Jijini Mbeya.
Amewataka wanachama wamuelewe hivyo ameona yeye akae pembeni badala ya
kuwa na muda mwingi wa kujadili migogoro ambayo haina tija na kuleta
mkanganyiko kwa wanachama.
Na Ezekiel Kamanga
Mbeya
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment