
Waandamanaji wa upinzani nchini Venezuela
Polisi nchini Venezuela
wamekabiliana na waandamanaji wa upinzani katika barabara za mji mkuu wa
Carcas ambao wanataka kuachiliwa huru kwa wanafunzi waliokamatwa wiki
iliopita.
Polisi wa kukabiliana na ghasia walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya huku waandamanaji hao wakiwatupia mawe.Rais Maduro ameushtumu upinzani kwa kuzua fujo kwa lengo la kutaka kuipindua serikali yake.
Watu watatu waliuawa wakati wa maandamano ya kuipinga serikali siku ya jumatano.
Waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani John Kerry ,ametoa taarifa akiitaka serikali ya bwana Maduro kuwaachilia huru wafungwa wote waliokuwa wakiandamana mbali na kuheshimu uhuru wa kujieleza.
>>>>>bbcswahili
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment