Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Maelfu ya watu walifika hospitali binafsi ya uzazi kwenye jiji la Kotaworo eneo la Bida, iliyopo jimbo la Niger jana Jumapili, kwa lengo la kwenda kumshuhudia mtoto wa kike aliyezaliwa akiwa amevaa Tasbihi shingoni mwake.


Inaelezwa kwamba mama wa mtoto huyo ambaye ana miaka ya kati, Adijat, alikimbizwa hospitali karibu na nyumbani kwa Pa Mohammed Bello Masaba, muda wa saa 8 mchana na baada ya pilika pilika za uzazi alifanikiwa kujifungua mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mmiliki wa hospitali hiyo ya uzazi, Alhaji Abubakar Baiwa Shasha ambaye ndiye aliyesimamia zoezi hilo la kujifungua alisema, “Nilishtuka nilipona mtoto anatoka akiwa na Tasbihi shingoni mwake, na wakati wa uzazi mtoto alizaliwa akiwa na Rozari nyeusi.” Alisema Shasha.

Ila nilishangaa baada ya muda rozari hiyo ilibadilika na kuwa nyeupe huku kukiwa na watu wengine wamezunguka.”

“Mara baada ya habari hiyo kusambaa mjini, maelfu ya watu walifika kwenye hospitali hiyo ya uzazi huku wakisema “Allahu Akibar; Allahu Akibar (Mungu ni Mkubwa) huku wakifika na kumgusa mtoto huyo.”

Juhudi za kumpata Baba wa mtoto huyo aitwaye Isah, ambaye anatokea eneo la Loma ndani ya Jimbo la Kwara State wzilishindikana baada ya kukataa kuongea na mtoa habari.

Mwanachuo mmoja wa Kiislamu, Malam Idiris Ndajiwo alisema, kuzaliwa kwa mtoto huyo akiwa na rozari “inaonyesha ukuu wa Allah. Kuzaliwa kwa mtoto huyu leo, kwenye mji huu na eneo hili (Kutaworo) ni kitu kikubwa kwa Waislamu. Hii hakika inakuja kuonyesha kwamba Allah ndiye mwenye kupanga kwa lolote kutokea kwa yeyote kwenye ulimwengu huu.”

                                   source DANCHIBO

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top