Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Umati wa watanzania waliojitokeza kuuaga mwili wa Mangwea jijini Dar es Salaam leo

WAKATI msarafa wa mwili wa aliyekuwa masanii wa muziki wa kizazi kipya,nchini Tanzanani marehemu Albert Mangwea ukielekea mjini Morogoro kwa mazishi, Rais wa Shirikisho la Muziki wa Kizazi kipya Tanzania (TMF) Addo November Mwasongo amezishambulia vyombo vya habari na kudai kwamba ziliandika vibaya taarifa za kifo cha msanii huyo.

Akizungumza wakati wa kusoma lisala ya TMF katika Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Mwasongo alisema kwamba, ”Tunalaani vikali vyombo vya habari vilivyokuwa vinaendelea kutoa habari ya kumchafua marehemu,tunasema huo si uungwana wala mila za kitanzania kumsema vibaya mtu ambaye hawezi kujibu(marehemu)tena kwa kutunga wakati hawajaiona ripoti ya daktari jambo hili halikubaliki hata siku moja”:.
"TMF ilipokea taarifa za kifo cha Mangwea kwa huzuni mkubwa sana na tukaungana na familia ya marehemu pamoja na watanzania wengine wakati huu wa msiba, Kamati hii pia inampa pole sana mwanamuziki Mgaza Pembe (M TO THE P) na kuwaomba watanzania tuzidi kumwombea mwanamuziki huyu mola amjalie afya njema na yenye baraka".
Mwasongo alisema kwamba TMF imewashukuru watanzania kwa kujitokeza kwa wingi na kuonyesha ushirikiano wao wakati wa msiba wa msanii huyo na kutoa heshima zao za mwisho wakati wa kuuaga mwili wake

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top