Mahabusu aliyekuwa akishikiliwa katika kituo kikuu cha polisi jijini Arusha aliyetambulika kwa jina la Victoria Wenga (51) mkazi wa Lemara jijini Arusha amejinyonga hadi kufa usiku wa kuamkia jana kwa kutumia shuka lake bila kuacha ujumbe wowote.
Marehemu alikamatwa Agosti 21 mwaka huu majira ya Alfajiri kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba yake na maduka yake mawili kutokana na ugomvi wa kifamilia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alikiri kutokea kwa tukio hilo katika Kituo cha Kikuu cha Polisi saa 6:20 usiku jana wakati wenzake wakiwa wamelala.
“Polisi wa zamu alisikia kelele kutoka kwenye chumba cha mahabusu wa kike ambapo polisi walijitahidi kuokoa maisha ya mahabusu huyo, lakini ilishindikanika,” alisema Kamanda Mkumbo.
Mahabusu huyo, ambaye ni mkazi wa Lemara jijini Arusha, alijinyonga kwa kutumia shuka lake alilokuwa anatumia kujifunikia wakati yuko mahabusi. Mtuhumiwa huyo, alijinyonga kabla ya kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka yake.
“Jana ilikuwa afikishwe mahakamani kujibu kosa lililokuwa linamkabili,”alisema Kamanda Mkumbo na kuwahakikishia kuwa hali ya usalama kituoni hapo na tukio hilo, havihusiani na sababu zozote za kiusalama.
Marehemu Victoria anadaiwa kuwa na ugomvi wa kifamilia na mume wake aliyetambulika kwa jina la Edward Wenga akimtuhumu kuzaa nje ya ndoa kinyume na utaratibu.
Imeelezwa kuwa hicho ndo chanzo cha marehemu kufikia hatua ya kuteketeza mali walizochuma na mume wake ambazo ni maduka mawili na nyumba ya kuishi.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuifadhia mahiti Hospitali ya Mount Meru.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment