Home
»
general news
» Kesi ya Mtanzania ( Rashidi Mberesero) Anayetuhumiwa Kwa Ugaidi Kenya Yaanza Kusikilizwa
Shahidi katika kesi ya shambulio la kigaidi lililofanyika mwaka jana katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya ameiambia mahakama kuwa Mtanzania Rashidi Mberesero anayetuhumiwa kushiriki, alikuwa akiswali katika msikiti ulio karibu na chuo hicho kwa siku tatu mfululizo.
Kolombo Adao ambaye ni imamu wa Msikiti wa Garissa alidai mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mlimani, Daniel Ogembo kuwa Mberesero aliondoka katika mazingira ya kutatanisha Aprili 2 mwaka jana huku akiacha begi lake msikitini.
“Alikuwa mwerevu mno na aliweza kuisoma Quran. Nilikutana naye mara ya kwanza asubuhi ya Machi 30, 2015 wakati nafungua msikiti,”alieleza shahidi huyo.
Kwa mujibu wa Adao, Mberesero alikuwa muumini wa kipekee kwani kila siku alikuwa akifika msikitini saa 10:35 alfajiri, wakati mwingine kabla ya adhana.
Shahidi huyo alidai kwamba Aprili Mosi mwaka jana alipofungua msikiti asubuhi alimkuta Mberesero akiwa ameshafika na alimpa kipaza sauti aweze kuwaita waumini wanaotakiwa kuswali asubuhi siku hiyo.
“Nilikuwa naumwa kifua siku hiyo. Kwa hiyo nilimpa kipaza sauti atangaze kwa sababu alikuwa anaijua vyema Quran,” shahidi huyo alidai.
Kuhusu sababu za Mberesero kuwapo Garissa, Adao aliiambia mahakama kuwa aliambiwa na kijana huyo kuwa alikwenda kumsalimia mjomba wake lakini alifukuzwa kwa kuwa ni Mwislamu.
“Alinieleza kuwa baba yake ni Mdigo wa Tanga na mama yake ni Mkamba wa Kenya,” alieleza Adao.
Kwa maelezo ya shahidi huyo, siku ya tukio Mberesero ambaye alizoea kuvaa kanzu alionekana amevaa mavazi ya kawaida na kofia kama mtu anayeficha uso.
Mahakama ilielezwa kuwa siku ya tukio aliingia msikitini na kuweka begi lake kwenye kona ya msikiti lakini hakusali na baadaye aliondoka na kuliacha.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Jamaa Aliyejitosa Zoo Aliwe na Simba Laivu Alikuwa Anadai Mwisho wa Dunia Umefika...23 May 20160
Inasikitisha kwakweli, ameokolewa.... na simba walioanza kumla waliuwawa. aliingia kwenye jumba ...Read more ?
- Watumishi HEWA Waziponza Benki.......Benki za Dar es Salaam Zalimwa Barua Kurejesha Mamilioni ya Shilingi23 May 20160
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa siku 21 kwa benki zilizokuwa zikitumika kuwek...Read more ?
- Waziri Nchemba Afanya Ziara Ya Kushtukiza Saa Saba Usiku Machinjio Ya Ukonga Mazizi Na Kufukuza Viongozi Wote Wa Machinjio12 Feb 20160
Waziri wa Kilimo na Mifugo Mwigulu Nchemba amefanya ziara ya Kushtukiza saa saba usiku...Read more ?
- Askofu Gwajima, Sheikh Wa Mkoa Dar Wakwama Kumjulia Hali Mufti12 Feb 20160
Jopo la Madaktari wanaomtibu Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir wamezuia ...Read more ?
- Siku 100 za Rais Magufuli: Hospitali Ya Muhimbili Yang'aa, Mapato Yapaa na Upatikanaji wa Dawa Waongezeka Kwa Asilimi 9611 Feb 20160
HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyopo jijini Dar es Salaam imesema ndani ya siku 100 z...Read more ?
- Lowassa Atakiwa Kuvisaidia Vyombo Vya Dola Kukabiliana na Tishio La Kundi la al Qaeda Kuingia Nchini10 Feb 20160
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amemtaka Wa...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment