Home
»
Stori muhimu
» Prof.Mwandosya: Magufuli Hajawahi Hata Kuwa Mjumbe wa Tawi la CCM...Iweje Apewe Urais Leo...
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Profesa Mark Mwandosya amethibitisha kuwa sauti iliyosambaa mitandaoni akieleza mtazamo wake juu ya mwenendo mzima wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM, ni sauti yake halisi.
Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania lililoongea naye, Mwandosya amethibitisha hayo akiwa katika harakati za safari yake ya kuelekea nchini India.
Katika sauti inayosikika kwenye mitandao, Profesa Mwandosya anasikika akieleza kuwa Kamati ya Usalama na Maadili iliendesha mchakato huo kinyume cha katiba kwa kuwa walikuwa na majina matano hata kabla ya kufanya usaili wao.
“Majina hayo matano ni ya January Makamba, Amina Salum Ali, Asha Rose Migiro, Bernard Membe na John Magufuli. Kilichotokea ni kitu cha ajabu kwa sababu majina hayo yalishatoka kabla hata kikao cha maadili hajikatoka, kinaendelea kikao majina sisi tunayo,” anasikika Mwandosya.
“Wanasema haya ndiyo yatakwenda mpaka mwisho, mmenielewa eeh, mfuatilie sana, mwenyekiti alikuwa na majina yake mfukoni na Kamati ya Maadili, Kamati Ndogo ya Maadili ina majina yake,” aliendelea Mwandosya.
Mwandosya alitoa maoni yake pia kuhusu uchaguzi wa Magufuli, na kudai kuwa mgombea huyo haifahamu vizuri CCM kwa kuwa hakuwahi kushika nyadhifa yoyote ya maana ndani ya chama hicho.
“Ni rafiki yangu Magufuli, lakini hajawahi kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama, hajawahi kuwa mjumbe hata wa tawi, hajawahi kuwa Mwenyekiti hata wa wilaya, CCM haijui, lakini sasa ndiye atakuwa mwenyekiti wa Chama cha Mampinzi, ndivyo chama kinavyokwenda.”
Mwandosya alisika akiponda mwenendo mzima wa kikao cha Halmashauri kuu baada ya kuyapata majina matano kwamba hakikuwa na mvuto na kwamba hata mwenyekiti wa chama hicho alikuwa anajichanganya.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- BREAKING NEWS: Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza rasmi tarehe ya kurudiwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar22 Jan 20160
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza rasmi tarehe ya kuru...Read more ?
- Rais Dkt. Magufuli Amteua Jakaya Kikwete Kuwa Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.21 Jan 20160
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa awamu ...Read more ?
- JANUARY MAKAMBAASHANGAZWA NA HAYA MAGAZETI MATATU KUHUSU LOWASSA02 Sep 20150
Naibu waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameonesha kushangazwa na mfa...Read more ?
- Polisi Yakamata Majambazi 38 Yakiwa na silaha Nzito pamoja na Milioni 170......Majambazi hayo yanadaiwa na mafunzo ya Kijeshi01 Sep 20150
Jeshi la Polisi limewakamata watu 38 wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi ambao pia wamepatiwa mafun...Read more ?
- Wananchi Wafunga Barabara Baada ya Gari la Polisi Kugonga Wanafunzi wawili31 Aug 20150
Wananchi wa eneo la Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani hii leo wamefunga barabara baada ya...Read more ?
- Hali Tete Bunda, Viongozi CHADEMA Wajiuzulu...Kisa Ester Bulaya22 Aug 20150
SIKU chache baada ya mgombea ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maend...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment