March 18, 2025 11:06:13 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Staa wa bongo movies,  Tamrina Posh ‘Amanda’ amesema kuwa  mfungo wa mwezi wa ramadhani umemuweka mbali na skendo ambazo amekuwa akiibuka nazo mara kwa mara  na ikiwezekana huo ndiyo utakuwa mwisho wake kwani kwa sasa yupo katika kipindui cha kuomba toba kwa muumba wake kwa mabaya yote  aliyowahi kufanya siku za nyuma.

Akizungumza na gazeti la Filamu, Amanda  alisema kwa mwezi  huu hatoonekana akikatiza mitaani na nguo zilizobana kiasi cha kuonyesha  maungo yake  ya sehemu za siri bali atakuwa anajisitili ili kujiepusha na kitendo cha kuwaingiza majaribuni wanaume hasa walio kwenye mfungo na mpaka mwezi huu unaisha atakuwa amezoea kuvaa nguo hizo.

“Naweza kusenma kuwa mfungo wa mwezio Ramadhani umeniweka kando na skendo  hasa za kuvaa nguo fupi ambazo huwa zinawaingiza  kwenye mitego  wanaume wasio weza kujizuia wanapoona maungo ya wanawake  hasa waliovaa nguo zenye ushawishi,” alisema Amanda.

Aidha, Amamnda aliwataka hata wasanii wenzake  hasa wa kike kuheshimu kipindi hiki kwani  ni  cha kuvuna neema  kutoka kwa Mungu kutokana na kutibu madhambi  yote yaliyofanyika siku za nyuma  na ikiwezekana na wao uwe mwanzo  wa kubadilishwa huhusu kuachana  na skendo za kujitakia  hasa zile za kutengeneza ili waendelee kusomeka kwenye magazeti

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
01 Jul 2015

Post a Comment

 
Top