Kwa mara ya kwanza, ‘mnyama’ katika anga la muziki wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed ‘Top In Dar’ (TID) amekiri kutumia mihadarati aina ya bangi huku akijiapiza kuwa hajawahi kutumia madawa mengine ya kulevya ‘unga’ ikiwemo cocaine kama ambavyo amekuwa akinyoshewa vidole na baadhi ya watu.
Akizungumza na Gazeti la Ijumaa katika mahojiano maalum wikiendi iliyopita, TID ambaye ni mmiliki wa Top Band alifunguka kuwa miongoni mwa mambo yanayomkosesha raha na amani ya moyo, ni pamoja na kuhukumiwa kujihusisha na matumizi ya unga na wengine kwenda mbele kwa kusema hata kushuka kwake kisanii kumechangiwa na ishu hiyo.
Staa huyo wa Ngoma ya Kiuno alisema kuwa, wakati mwingine watu wanamsakama hadi mama yake mzazi wakimtaka amkanye mwanaye kujiepusha na maisha ya ‘kubwia unga’ jambo ambalo linampa wakati mgumu na kujiona kuonewa katika jamii.
Kuhusu kushuka kimuziki, TID alisema miongoni mwa sababu zilizosababisha kuporomoka katika anga la muziki ni kile alichokiita ‘hujuma’ kutoka kwa baadhi ya wadau wakubwa wa muziki (majina yapo), kwa kushindwa kumpa fursa za kimuziki zikiwemo promosheni na mialiko ya shoo kwa kuwa wana vinyongo na fitina dhidi yake.
“Kaka, naonewa kabisa nikihusishwa natumia madawa ya kulevya, wanamsumbua mama eti akae na mimi anionye.
“Jamani situmii madawa ya kulevya kama cocaine, ila kwa upande wa bangi ni sawa nakubali kuwa navuta.
“Lakini pia, kuvuta kwangu bangi siyo sababu ya mimi kushuka kisanii, zipo sababu zingine kabisa kama kuhujumiwa na wadau wakubwa wa soko la muziki kutokana na mabifu yanayotokana na sababu binafsi.
“Hivi kweli mtu anayetumia madawa ya kulevya kama cocaine, anaweza kumudu maisha kama kununua nyumba? Kununua magari? Hata kuendelea kuimba kweli? Siyo sawa jamani,” alisema TID.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Diamond kuwania tuzo 5 za Afrima 2016, Alikiba na Yamoto Band moja08 Sep 20160
Diamond Platnumz ametajwa kuwania vipengele vitano kwenye tuzo za mwaka huu za Afrima. Vipeng...Read more ?
- Ujumbe wa Diamond kwa bintiye Wazua Gumzo......Kamwambia "Ukikua chonde mama ukitunze wasikile sana"23 Jul 20160
Diamond Platnumz si mgeni kwenye jumbe tata kwenye mitandao ya kijamii. Lakini ujumbe wake mpya...Read more ?
- Bifu Kali Kati ya Diamond na Clouds Media23 May 20160
Ni dhahiri sasa msanii wa kimataifa Diamond na brand kubwa ya radio na tv Clouds Fm, bifu la hadh...Read more ?
- Afande Sele Aungana Na Mbunge Joseph Msukuma Kuitaka Serikali Ihalalishe Matumizi Ya Bhangi02 Feb 20160
Msanii mkongwe wa hip hop nchini, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumiz...Read more ?
- Gari Jipya Analomiliki Masanja Mkandamizaji.10 Jan 20160
Msanii wa Vichekesho Anawakilisha kundi la Orijino Komedi anayejulikana kama Masanja Mkand...Read more ?
- Zari The Lady Boss Awakosha Mashabiki wa Penzi lake na Diamond Kwa Picha Hizi09 Jan 20160
Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ amewakosha mashabiki wa penzi lake na Diamond ‘Baba Tiffah’ baada...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment