Home
»
wema sepetu
» Wema Sepetu Katika Shutuma ya Kusambalatisha Ndoa ya Dada Yake Diamond Esma Platnumz na Meneja Wake Petit Man.
Hatimaye lile sekeseke la ndoa ya meneja wa wasanii wa Bongo Fleva wanaosimamiwa na Kampuni ya Endless Fame, Petit Man na mdogo wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Platnumz limemdondokea Wema Isaac Sepetu anayedaiwa kuitibua kiasi cha kuwatenganisha na kila mmoja kuchukua hamsini zake.
Habari kutoka chanzo chetu zilidai kwamba, Wema amehusika kwa asilimia kubwa kutibua ndoa hiyo kwani amekuwa akimtafutia mademu Petit Man, jambo ambalo Esma alilishtukia na kuamua kumbwatukia Wema kwa kuandika maneno makali kwenye mitandao ya kijamii.
“Kwa taarifa yenu Esma anamlalamikia Wema kuwa anamfanya mumewe kuwa mhuni kiasi kwamba anachukua mademu, tena marafiki zake na hata akimuuliza Petit Man anajifanya hao ni mashoga wa Wema.“Anapomkomalia, mara kadhaa umekuwa ukizuka ugomvi mkubwa na Petit Man anahama nyumbani kwake na kukimbilia kwa Wema,” kilisema chanzo chetu.Baada ya kunyetishiwa ‘infomesheni’ hizo, gazeti hili liliingia kazini kusaka ukweli wa mambo yanayodaiwa juu ya
lilianzia kwa Esma, alipopatikana alisema ni kweli hivi karibuni aliandika ujumbe kwenye Mtandao wa Instagram, ingawa kwenye maelezo yake hakumtaja mtu bali aliandika kwa hisia kama binadamu mwingine anavyoweza kuandika.
“Nani anasema nimemtukana mtu? Niliandika mambo ambayo nilijisikia mwenyewe lakini sikumtaja wala kumlenga mtu yeyote, kama kuna mtu alikwazika basi atakuwa anajichanganya mwenyewe.“Mimi sina tatizo na Wema na mambo ya familia yangu siwezi kumwambia kila mtu hivyo kama kuna ugomvi kati yangu na mume wangu hayo ni mambo ya familia yetu,” alisema Esma.
Kwa upande wake Wema alifunguka kwamba hajawahi kuongea jambo na Esma na kama kuna kitu aliandika kwenye ‘peji’ yake yeye hakuona.Alisema anachokumbuka ni kwamba aliongea naye (Esma) akiwa Hospitali ya Aga Khan Aghakan, Dar.
“Huwa siongei na Esma mara kwa mara kwani sina sababu sana ya kuwa naye kwa kuwa si mume wala bwana’ngu.
“Pia sijawahi kukwaruzana naye, sasa kama kuna kitu alisema, mimi namtafutia wanawake mumewe basi atakuwa anakosea kabisa,” alisema Wema.
>>>>>GPL
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- VIDEO: Mama Wema Aeleza Beef yake na Man Fongo Kisa……..09 Sep 20160
NI Mama Wema Sepetu ambae ameingia kwenye headlines mitandaoni baada ya kutofautiana na mkali wa ...Read more ?
- Wema Sepetu ampigia magoti Idris Sultan22 Aug 20160
Uhusiano wa Wema Sepetu na Idris Sultan unaanza kutukumbusha ule wa Chris Brown na Karrueche Tr...Read more ?
- Wema Sepetu: Niacheni jamani Nimechoka03 Aug 20160
Wema Sepetu Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu ameonesha kuchoka na maneno mbalimbali k...Read more ?
- Idris Sultan Amtundika Mimba Wema Sepetu25 Jan 20160
Mshindi wa Big Brother Afrika, Idris Sultan amepasua jipu kuhusu uhusiano wake na Wema Sepetu...Read more ?
- Kipindupindu Chanyemelea Nyumbani Kwa Wema Sepetu28 Aug 20150
Mrembo Wema Sepetu Taarifa za ugonjwa wa kipindupindu zimebadili mfumo wa maisha ya watu wengi i...Read more ?
- Wema Sepetu na Lowassa ni 'Paka na Chui'......Atoa ONYO Kali Kwa Team Wema11 Aug 20150
Kama unamfatilia Wema Sepetu kwenye mitandao yake ya kijamii jana kupitia mtandao wa Instagram a...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment