Home
»
general news
» Mchungaji Mbaroni kwa Kumchinja Mwanaye Adai "Nilioteshwa na Mungu, Mkuu wa majeshi Nimtoe Sadaka"
DUNIA ina mambo! Mchungaji wa kanisa moja mjini Harare nchini Zimbabwe, ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, amekamatwa na polisi baada ya kukutwa akitaka kumuua mwanaye wa kumzaa kwa kumchinja na kisu shingoni, kitendo alichokifanya nyumbani kwake mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mchungaji huyo ambaye hata hivyo hakueleweka ni wa kanisa gani, akiwa amevaa nguo zake za kichungaji, kanzu nyeupe yenye msalaba kifuani, alimchukua mwanaye huyo wa kiume na kuanza kumchinja ndani ya nyumba yake, kabla ya kijana huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kumi, kupiga kelele za kuomba msaada.
Kwa mujibu wa mitandao, baada ya majirani kuingia ndani ya nyumba hiyo, walimkuta mchungaji huyo akiwa na kisu mkononi, ameloa damu huku kijana wake akiwa ameanguka chini akiugulia kwa maumivu makali.
Baada ya kuhojiwa sababu za kutaka kutoa roho ya mwanaye, mchungaji huyo alitoa majibu ya kushangaza;
“Nilioteshwa na Mungu, Mkuu wa majeshi. Alinitaka kumtoa sadaka mtoto wangu kama kweli nilikuwa na imani naye, sasa kwa sababu kila siku hufanya mambo yangu kwa kusikia sauti yake, nikaifuatisha. Ni kama Ibrahim alivyofanya katika Biblia.”
Hata hivyo, imeelezwa kuwa kijana huyo alikuwa bado hajafariki na aliwahishwa hospitalini ambako anaendelea na matibabu wakati mchungaji huyo ameendelea kuwa mikononi mwa polisi ambao wanamhoji kabla ya kufikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Jamaa Aliyejitosa Zoo Aliwe na Simba Laivu Alikuwa Anadai Mwisho wa Dunia Umefika...23 May 20160
Inasikitisha kwakweli, ameokolewa.... na simba walioanza kumla waliuwawa. aliingia kwenye jumba ...Read more ?
- Watumishi HEWA Waziponza Benki.......Benki za Dar es Salaam Zalimwa Barua Kurejesha Mamilioni ya Shilingi23 May 20160
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa siku 21 kwa benki zilizokuwa zikitumika kuwek...Read more ?
- Waziri Nchemba Afanya Ziara Ya Kushtukiza Saa Saba Usiku Machinjio Ya Ukonga Mazizi Na Kufukuza Viongozi Wote Wa Machinjio12 Feb 20160
Waziri wa Kilimo na Mifugo Mwigulu Nchemba amefanya ziara ya Kushtukiza saa saba usiku...Read more ?
- Askofu Gwajima, Sheikh Wa Mkoa Dar Wakwama Kumjulia Hali Mufti12 Feb 20160
Jopo la Madaktari wanaomtibu Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir wamezuia ...Read more ?
- Siku 100 za Rais Magufuli: Hospitali Ya Muhimbili Yang'aa, Mapato Yapaa na Upatikanaji wa Dawa Waongezeka Kwa Asilimi 9611 Feb 20160
HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyopo jijini Dar es Salaam imesema ndani ya siku 100 z...Read more ?
- Lowassa Atakiwa Kuvisaidia Vyombo Vya Dola Kukabiliana na Tishio La Kundi la al Qaeda Kuingia Nchini10 Feb 20160
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amemtaka Wa...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment