RAPPA, komedian na mwigizaji wa Marekani, Nicholas Scott "Nick" Cannon ameamua kumfutilia mbali mkewe wa zamani Mariah Carey kwa tattoo nyingine zaidi mgongoni mwake.
Awali Nick Cannon (34) aliamua kufuta tattoo ya jina la mkewe Mariah Carey aliyeachana naye mwaka jana kwa tattoo ya mchoro wa Yesu akiwa msalabani.
Kuona kuwa hiyo haitosha, staa huyo ameamua kuongeza tattoo zaidi ili kumwondoa kabisa mkewe huyo akilini ambapo ameongeza michoro mingine mgongoni ikiambatana na maneno haya kwa chini "Baba, wasamehe watu hawa maana hawajui walifanyalo" maneno ambayo yatakuwa yanahusiana na ndoa yake na Mariah.
Cannon na Mariah walifunga ndoa mwaka 2008 na kudumu kwa miaka sita kabla ya kuachana mwaka jana.
Katika mahusiano yao walifanikiwa kupata watoto wawili mapacha Monroe na Moroccan.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment