Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Kijana mwenye tatizo la ulemavu amegundulika kufungiwa ndani ya chumba kwa zaidi ya miaka kumi na wazazi wake kwa madai ya kuficha aibu bila kutolewa nje kupata hewa katika chumba kilichopo mtaa wa uwazi kata ya kangarawe wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.

ITV ilifanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo kabla ya kwenda na camera yao na kuakikisha kuwa kijana huyo ambaye amejulika kwa jina la Hamza Abdalah mwenye umri wa miaka 22 akiwa katika chumba hicho kwa zaidi ya miaka kumi bila kutolewa nje huku akijisaidia katika chumba hicho ambapo licha ya baadhi ya viongozi wa mtaa huo kupata taarifa hizo, wamelalamikia wazazi wa kijana huyo kwa kuficha ugonjwa wa mtoto wao kwa zaidi ya miaka 10 bila kuweka wazi ili jamii iweze kusaidia.
 
ITV ilipoonana na wazazi wa kijana huyo bwana Abdalah Amri na mkewe, walikiri kumfungia kijana wao kwa miaka mingi, huku wakijitetea kuwa wameishiwa fedha kutokana na matibabu yake.
 
Aidha viongozi hao pamoja na timu ya ITV tulilazimika kumtoa kijana huyo nje ili aweze apate hewa kuliko kuendelea kukaa katika chumba hicho chenye harufu mbaya. 

Chanzo: ITV

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
28 Mar 2015

Post a Comment

 
Top